Tuesday 30 June 2015

MAANDALIZI YA MUHULA MPYA 2015
Malengo yetu bado yanasimama palepale kuwa ni kuhakikisha tunafanya vizuri kwa mitihani ya ndani pamoja na mitihani ya mwisho ya taifa kwa kidato cha nne,hivyo sisi kama Kikanda sekondari tumejiandaa vya kutosha ili kutoa elimu iliyo bora na inayokidhi mahitaji ya jamii yetu ya Kitanzania kutokana na mwongozo wa mtaala wetu.Kama isemavyo ratiba tunategemea kufungua shule tarehe 13/07/2015 hivyo tunaomba wazazi pamoja na walezi wa wanafunzi wa  Kikanda Sekondari kuhimiza vijana wao kuwahi shule ili wasipitwe na masomo ambayo yamepangwa kwa mujibu wa ratiba.

WAZAZI
WAZAZI
ZINGATIA-mzazi unapaswa kumueleza kijana wako umuhimu wa elimu na kuwa na nidhamu bora katika kipindi chote atakachokuwa shuleni

RATIBA YA MUHULA
Tunategemea kuweka ratiba ya muhula mzima kutoka kufinguliwa shula mwezi ujao mpaka kufungwa hapo baadae mwezi wa 12 /2015 ili kusaidia wewe mzazi na mwanafunzi kuweza kufahamu ratiba nzima ya masomo
Ahsanteni

MENGINEYO
Endelea kutufuatilia hapa Kikandasecondary.blogspot.com,facebook.com.au twitter.com  ili uweze kupata ratiba zetu,matokeo ya mitihani yetu ya ndani kama weekly test na mid term test.Michezo mbalimbali na shughuli nyinginezo za shule katika muhula huu mpya.
Natanguliza shukurani

Mkuu wa Shule>Kikanda sekondari-Kilwa

No comments :

Post a Comment

Tricks and Tips